Thursday, April 26, 2012

Washington, Marekani - 17/04/2012. Wachunguzi wa mambo ya kisiasa nchini Marekani wametoa matokeo ya utafiti wa kura za maoni wa ugombea urais ambao unaonyesha rais wa sasa Baraka Obama  anaongoza.
Kwa mujibu wa kura hizo za maoni, "Baraka Obama  wa chama cha Demokratic anaongoza kwa  52% na mpinzani wake Mitt Romney wa chama cha Republikan  kupata kura za maoni  43%." na wanacha wa chama Demokratik  kudai ya kuwa  Baraka Obama  ndiye kiongozi anayefaa kuingoza tena Marekani.
Matokeo hayo yamekuja baada ya  mgombea mwenza wa chama cha Republikan Rick Santorum kujitoa katika kinyang'anyiro cha kugombe kiti cha urais wa Mareakani na kumwachia nafasi mgombea pekee  kupitia chama hicho Mitt Romney.  
Pilika za kutaka kuwania kiti cha urais nchini Marekani zimeshaaanza kwa mwendo wa gia namba moja tayari kwa kila mgombea kujipanga wakati wa safari hiyo ndefu ya kutaka kuingia Ikulu ya Marekani.

No comments: