Thursday, April 26, 2012

KAIRO

Kairo, Misri - 23/04/2012. Shirika linalo sambaza na mushughulikia masi nchini Misri limetangaza kusimamisha uuzaji wa gasi nchi Izrael kuanzai sasa.
Mohamed Shoeb ambaye ni msemaji wa kampuni ya usambazaji gasi nchini Misri - Egypt Natural Gas Company alisema " tumeamua kusimamisha uuzaji wa gasi nchini Izrael na uamuzi huo ni wa kibiashara na wala si wakisiasa."
Waziri wa fedha wa Izrael Yuval Steinitz alisema " uamuzi wa Misri kusimamisha uuzaji wa gasi ni wa kuangaliwa kwa makini kisiasa na kiuchumi.
"Hii ni hatari kwani kunakiuka mkataba wa amani na utulivu iliyopo kati ya Izreal na Misri na uamuzi huo siyo mzuri na haufai."
Swala la uuzaji wa gasi kati ya Misri na Izrael uliingia dosari mara baada ya kuangushwa serikali ya rais Husni Mubaraka, ambapo serikali yake ilikuwa na mawasiliano mazuri na serikali ya Izreal tangu achukue madaraka ya urais 1981.


No comments: