Wednesday, May 9, 2012

BASI LA ABIRIA LATEKETEA!

Basi la kampuni ya Muro Investment, lenye namba za usajili T820BEY lillilokuwa likitokea Mwanza kwenda jijini Dar es Salaam, limewaka moto na kuteketea  kabisa maeneo ya Maseyu, Mkoani Morogoro. Ajali hiyo iliyotokea majira ya saa 1:15 usiku  wa Mei 8, 2012, haikusababisha madhara kwa abiria isipokuwa mali zao zote ziliteketea kwa moto
 Magari yakipita pembeni ya basi hilo lililokuwa likiteketea kwa moto na hapakuwa na askari wala magari ya zima moto yaliyoweza kuwahi kufika na kuzima moto huo ulioliteketeza basi hilo…

No comments: