Thursday, September 6, 2012

Here steve Jobs History..http://en.wikipedia.org/wiki/Steve_Jobs

 Shoulder-high portrait of smiling man in his fifties wearing a black turtle neck shirt with a day-old beard holding a phone facing the viewer in his left handhttp://en.wikipedia.org/wiki/Steve_Jobs

Democratic convention: Obama lays out election choice


Barack Obama spoke of the challenges ahead in his closing speech at the Democratic National Convention
US President Barack Obama has accepted the nomination of the Democratic party, telling voters they face a generational choice in November's election.
He highlighted the differences between his aims and Republican policies, and reprised his 2008 theme of "hope".
"I never said this journey would be easy, and I won't promise that now," Mr Obama told the Democratic convention.
Republican Mitt Romney is challenging Mr Obama for the White House, with polls showing a tight race.
Mr Obama told delegates in the hall and voters watching at home that the nations problems have built up over "decades" and cannot be fixed in a flash.

Start Quote

From all that we've seen and heard, they want to take us back to an era of blustering and blundering that cost America so dearly”
Barack ObamaUS President
"But when you pick up that ballot to vote - you will face the clearest choice of any time in a generation.

"Over the next few years, big decisions will be made in Washington: on jobs and the economy; taxes and deficits; energy and education; war and peace - decisions that will have a huge impact on our lives and our children's lives for decades to come," he said.

Dotynta Amvuta Kaseba.


Husna Poshi 'Dotnata'
MWIGIZAJI na mtayarishaji wa filamu za Swahiliwood, Husna Poshi 'Dotnata', yupo katika maandalizi ya filamu mpya ambayo ameshirikiana na mpiganaji wa ngumi za mateke, Japhet Kaseba pamoja na mkewe.

"Ni filamu ya kipekee, itakuwa bomba sana wenyewe mtaikubali," alisema Dotnata.

"Ni kweli mara nyingi watu wanaandaa filamu za mapigano lakini kuna sehemu zinakosewa kwani huwa zinatumia upiganaji wa kifilamu.

"Lakini katika kazi hiyo mpya mtakutana na mtu mwenye fani yake. Kwa kilichofanyika mpaka sasa ninajivunia ubora wa filamu hiyo.

"Siitaji jina kwa sasa, lakini mtaipata muda si mrefu ujao, kaeni mkao wa kula."

Kaseba ni mpinzani mkubwa wa bongia mwingine wa ngumi za mateke, Seba, ambaye yeye aliingia katika tasnia ya filamu kitambo.

Akizungumzia hilo, Kaseba, amesema alikuwa akisita kuingia katika filamu kutokana na fani hiyo kuwa chini mno nchini, lakini sasa ameridhika kuwa angalau inapiga hatua.

Saturday, July 14, 2012

End of Facebook{15 july 2012}

 Facebook continues to deny rumors it is shutting down on July 15th of 2012. WWN, however, has confirmed that it is true.

On January 9th, WWN’s ace reporter, J.B. Smitts, broke the international story that Facebook was going to close down on July 15th because Mark Zuckerberg wanted to return to a normal life. The story caused a worldwide sensation, and J.B. Smitts has been nominated for a Pulitzer Prize for breaking it.

READ WWN’s ORIGINAL FACEBOOK STORY

Facebook COO, Sheryl Sandberg has publicly denied the rumors, saying, “Facebook is not going to close down. Not now, not ever. We’re just getting started.”

David Ebersman, the CFO of Facebook, and the man working with Goldman Sachs on the new Facebook financing deal said, “many people feel that the deal with Goldman Sachs will lead to a change in Facebook or that we might shut down so the government won’t force us to go public. All of those rumors are false. We are going to be stronger than ever after July 15th.”

But WWN has spoken to insiders at Facebook who strongly contradict the public statements of the executive management team.



Sources inside Facebook tell us that the company is already making plans on how to handle the big shutdown. “We can’t just turn it off on July 15th of 2012. There will be a revolution,” said one insider. “We have to prepare our users for the end of Facebook and offer them ways to keep their social networks alive.”

Zuckerberg maintains that one year is enough time for users to prepare for the demise of Facebook. It also gives rival sites time to build up their user base.

There were rumors that Zuckerberg himself was going to appear on the Oscars or a the Super Bowl, but Zuckerberg did not show up at either event. New rumors are that Zuckerberg will make “an important announcement to the world” about the future of Facebook when he meets with President Obama in the White House on June 15th.

Meanwhile, there is panic all around the globe as Facebook users (and addicts) are frightened that they may lose their social networking community. Top celebrities Tyra Banks, Mila Kunis, Britney Spears, Lady Gaga, Justin Beiber, Ashton Kutchter, Carrot Top, Meryl Streep, Danny Bonaduce and the Real Housewives of New Jersey and Atlanta are all panicking about losing Facebook. “I’m addicted to Facebook,” said Tyra Banks. “Without it, my life is over!”



An online petition was started just hours ago to help persuade Zuckerberg and Facebook to remain open.

SIGN THE “SAVE FACEBOOK” PETITION HERE.

The organizer of the “Please Do Not Shut Down Facebook Petition”, Fritz Barnkopf, said, “we hope to get a million or more signatures before the Oscars, so Mark Zuckerberg will reconsider his tragic decision.”

WWN is following this developing story closely – constantly talking with Facebook insiders. We certainly are rooting for Facebook to continue because it’s an important part of our own social media strategy and leading source for our site visits.

WWN is your only reliable news source on this – and all – breaking news stories.

And now… one of the MANY videos from panicked Facebook users about the shut down:

Friday, July 13, 2012

kocha awapa adhabu chuji na tegete..

KAMA nyota wa Yanga walidhani ujio wa kocha mpya, Tom Saintfiet, utakuwa starehe tupu wamejidanganya kwani Jerry Tegete na Athumani Iddi Chuji wamekuwa wa kwanza kuonja joto ya jiwe ya Mzungu huyo kwenye mazoezi ya jana Jumatatu.

Mbelgiji huyo alidhihirisha si mtu wa mzaha baada ya kutoa adhabu ya kupiga `push up' 10 kwa kila mmoja wa wawili wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika Uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Saintfiet alikasirishwa na kitendo cha nyota hao kutokuwa makini kwenye mazoezi.
Baada ya kuwaadhibu akina Chuji, Saintfiet aliwaambia wachezaji kutofanya mzaha wakati wa mazoezi na kuwataka wawe wakakamavu na makini wakati wote kama wanajeshi.

"Ninataka kila mchezaji afuatilie kwa makini mazoezi na hii yote ni kwa manufaa ya timu. Hakuna mtu, ambaye yuko juu ya timu. Muwe kama wanajeshi," alisikika Saintfiet akiwaambia wachezaji hao wakati wa mazoezi hayo.

Katika hatua nyingine, Mnyarwanda Haruna Niyonzima amekoshwa na staili ya ufundishaji wa kocha huyo.

�Kila mchezaji amefurahishwa na staili ya ufundishaji wa Saintfiet, nafikiri tumepata bonge la kocha, naamini ataibadilisha Yanga na kucheza soka la kisasa,� alisema Niyonzima.

Saturday, June 30, 2012

Pinda: Tunachunguza bilioni 300 za Uswisi



 WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema Serikali kupitia vyombo vyake vya dola, imeanza kuchunguza taarifa za kuwapo kwa Sh300 bilioni zilizofichwa nchini Uswisi.Pinda aliliambia Bunge jana kuwa, Serikali pia ilisoma taarifa kwenye vyombo vya habari kama walivyosoma wabunge, na kwamba tayari wameanza uchunguzi kuhusu suala hilo na baada ya uchunguzi matokeo yatatangazwa.

Alivitaja vyombo vinavyochunguza tuhuma hizo kuwa ni Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Taasisi ya Kuchunguza na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Kitengo cha Kiiteliejensia cha Wizara ya Fedha (Fiu).

Pinda aliyasema hayo jana wakati akijibu hoja za baadhi ya wabunge, ambao katika kuchangia bajeti ya Waziri Mkuu walitaka kupewa maelezo ya kutoroshwa kwa fedha hizo.

Taarifa za kufichwa kwa fedha hizo kwenye akaunti sita za wanasiasa na vigogo wa Serikali, ziliripotiwa wiki iliyopita na magazeti ya Mwananchi na The Citizen pekee, zikinukuu ripoti ya Benki ya Taifa ya Uswisi (SNB), iliyotolewa hivi karibuni, ikitaja nchi mbalimbali ikiwamo Tanzania, na kiwango cha fedha zilizohifadhiwa huko.
Mbali ya Tanzania, nchi nyingine ambazo zina fedha nyingi katika benki za Uswisi ni Kenya (Dola 857 milioni), Uganda (Dola 159 milioni), Rwanda (Dola 29.7 milioni) na Burundi Dola 16.7 milioni.

Chanzo cha habari hizo kilieleza kuwa, tangu akaunti hizo zifunguliwe na kampuni za kuchimba mafuta na madini, wamiliki wake halali kutoka hapa nchini, hawajawahi kuingiza hata shilingi moja.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, akichangia bajeti ya Waziri Mkuu, aliitaka Serikali kuchunguza, kuwataja na kuwachukulia hatua wamiliki wa akaunti hizo.
 
Alisema, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ielekezwe ili ifanye uchunguzi utakaowezesha wamiliki wa akaunti zao kufahamika ili wachukuliwe hatua mara moja bila kujali nafasi wanazozishika serikalini.

Jana akijibu hoja za wabunge, Pinda alisema: “Serikali kupitia vyombo vyake (Takukuru, Financial Intelligency Unit (Fiu) wameanza kufanya uchunguzi wa taarifa hizo kwa kuzingatia taratibu za kisheria.”

Pinda pia alionya ukiukwaji wa makusudi wa sheria, taratibu na miongozo mbalimbali ya Serikali, unaofanywa na baadhi ya viongozi wa Serikali wasio waaminifu wakati wa kutekeleza majukumu yao.
“Kwa kweli hatuwezi kuendelea kuvumilia hali hiyo, na sisi tunasema wabunge kupitia kamati zetu zile tatu za masuala ya fedha na kamati nyingine za kisekta mnatusaidia sana maana lazima tubadilike ili tuweze kutoka hapa tulipo,”alisema Pinda.

Pinda alisema Serikali haijalifumbia macho suala hilo na kwamba hatua stahiki za kinidhamu zimekuwa zikichukuliwa kwa viongozi na watendaji wa aina hiyo kila walipobainika.

“Mathalan katika kipindi cha mwaka 2011/2012 wakurugenzi wapatao 48 walichukuliwa hatua za kinidhamu au kufikishwa mahakamani kwa makosa mbalimbali ya kinidhamu ikiwa ni pamoja na vitendo vya wizi, rushwa, ubadhirifu, ukiukaji wa maadili na kushindwa kutekeleza majukumu yao,” alisema Pinda.
Pinda pia alizungumzia kwa undani mgawanyo wa fedha za rada zilizorejeshwa kutoka Uingereza, maarufu kama chenji ya rada, kuwa zitatumika kwa ununuzi wa vitabu na madawati, kwa kuwa ndiyo makubaliano yaliyofikiwa na pande husika.

Pande hizo ni Serikali kupitia Wizara ya Fedha, wakati Uingereza iliwakilishwa na DFID, BAE Systems na SFO.

“Matumizi ya fedha hizo yanalenga kuimarisha uendeshaji wa Elimu ya Msingi ambapo asilimia 75 ya fedha zitatumika kununua vitabu vya kiada, vitabu vya mwongozo kwa walimu, mihutasari na miongozo ya mihutasari, asilimia 25 itatumika kununua madawati,” alisema Pinda.
Alisema vitabu hivyo vitanunuliwa kutoka kampuni 13 za wachapishaji zilizoteuliwa ambazo, ni Ben Company, Best Deal Publisher, E & D Vision, Education Books Publisher, Jadida, LongHorn, Longman, Macmillan, Mkuki na Nyota, Mture, Oxford, Taasisi ya Elimu Tanzania na Ujuzi Book.

Pinda aliongeza kuwa kati ya kampuni hizo, kinyume na ilivyodaiwa na baadhi ya wabunge, mbili tu ndiyo za nje, lakini zina matawi hapa nchini na kwamba kampuni nyingine zilizobaki wamiliki wake ni Watanzania.

Daktari: Hali ya Ulimboka mbaya


Mgonjwa akiwa nje ya geti la Taasisi ya Mifupa MOI jijini Dar es Salaam jana akiwa ajui chakufanya baada kukuta geti hilo limefungwa kutokana na mgomo wa madaktari unaoendelea nchini.Picha na Venance Nestory
ASEMA FIGO ZAKE ZIMESHINDWA KAZI, ZATAKIWA DOLA 40,000 KUMPELEKA INDIA
Geofrey Nyang’oro na James Magai
AFYA ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka imebadilika na kuwa mbaya, baada ya figo zake kushindwa kufanya kazi ya kuchuja sumu ya mwili na kusababisha apatiwe huduma ya kusafisha damu yake.

Habari zilizopatikana jana na kuthibitishwa na kiongozi wa jopo la madaktari wanaoendelea kumtibu, Profesa Joseph Kahamba, zilieleza kuwa hali ya Dk Ulimboka ilibadilika na kuwa mbaya na hivyo kuwapo mikakati wa madaktari wenzake kukusanya fedha ili kumpeleka nje ya nchi.

Dk Ulimboka ambaye amelazwa katika Kitengo cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalumu (ICU) katika Taasisi ya Mifupa (MOI), alipatiwa huduma hiyo jana asubuhi kwa kutumia mashine maalumu, iliyoko katika Kitengo cha Watoto cha Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

Daktari huyo ambaye alikuwa anaratibu mgomo wa madaktari unaoendelea nchi nzima kutokana na Serikali kushindwa kutimiza madai yao mbalimbali, amelazwa kutokana na majereha aliyoyapata katika sehemu mbalimbali za mwili, baada ya kutekwa na watu wasiojulikana, kisha kupigwa, kung'olewa kucha, meno mawili na kutupwa katika Msitu wa Pande, usiku wa kuamkia Jumatano.

Tangu alazwe MOI baada ya kuokotwa na wasamalia wema, katika Msitu wa Pande uliopo nje kidogo ya Jiji la Dares Salaam, hali ya afya ya Dk Ulimboka imekuwa tete na jana ilizidi kuwa mbaya.

Kauli ya Dk Kahamba

Akizungumza na gazeti hili jana, Profesa Kahamba alisema kutokana na tatizo hilo, mgonjwa huyo jana alilazimika kusafishwa damu.

Alieleza hayo alipotakiwa kuthibitisha taarifa zilizolifikia gazeti hili kuwa afya ya Dk Ulimboka haikuwa nzuri na madaktari wanachangishana fedha kumpeleka kwenye matatibu ya kusafishwa damu katika Hospitali ya Regency jijini Dar es Salaam au nje ya nchi.

"Taarifa hizo zina ukweli, lakini siyo jambo rahisi kiasi hicho kwamba anatakiwa kusafishwa damu. Kama ni damu amesafishwa leo (jana) asubuhi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili," alisema Profesa Kahamba na kuendelea:

"Suala lake ni complicated (tata) zaidi, lakini ili watu waelewe, siyo mbaya mkisema figo zimefeli(zimeshindwa kufanya kazi)."

Alipotakiwa kueleza sababu ya tatizo hilo, Profesa Kahamba alisema, "Siwezi kueleza kwa undani ila haya maumivu ya kupigwa na kuteswa yanachangia kwa kiasi kikubwa."

Alipotakiwa kueleza yeye anaonaje hali ya sasa ya Dk Ulimboka, Profesa Kahamba alisema: “Ni uongo tukisema anaendelea vizuri."

Aliendelea, "Unajua alipofikishwa hapa Muhimbili juzi (Jumatano) afya yake ilikuwa mbaya, na jana (Alhamisi) alionekana kuendelea vizuri, lakini jana hiyohiyo, hali yake ilianza kubadilika na vipimo vilionyesha kuwa ana complications (matatizo) za figo.

"Sasa figo ni kitu sensitive (muhimu) sana, anahitaji uangalizi wa karibu na kimsingi hatuwezi kusema kwamba anaendelea vizuri. Ni vyema tukisema tu afya yake ni mbaya," alieleza.

Taarifa za awali kutoka kwenye chanzo chetu hospitalini hapo, zilieleza kuwa Dk Ulimboka ambaye alipata tatizo linalojulikana kama “Acute renal failure”, alifanyiwa tiba inayojulikana kama Dialysis, ambayo ni kitendo kutumia mashine maalumu kufanya kazi ya kuchuja sumu ya mwili kwenda kwenye mkojo, baada ya figo ambazo hufanya kazi hiyo kushindwa.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, Dialysis inaweza kumsadia mgonjwa ambaye figo zake zimeshindwa kufanya kazi, kuishi kama kawaida, lakini kwa Dk Ulimboka haikutoa matokeo mazuri.

Michango ya madaktari

Jana ulifanyika Mkutano wa Madaktari Bingwa wa MNH, Chuo Kikuu Sayansi ya Tiba Muhimbili (MUHAS) na Ocean Road (ORCI) na kuazimia kukusanya Dola za Marekani 40,000 (Sh64,000,000) ili Dk Ulimboka asafirishwe kwenda India kwa matibabu zaidi.

Taarifa za maazimio hayo zilitangazwa kwa waandishi wa habari na Katibu wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Edwin Chitega, kuwa afya ya Dk Ulimboka haikuwa nzuri hivyo zikipatikana fedha hizo angepelekwa nje ya nchi.

Dk Chitega aliwataka wanataaluma hao na wananchi kwa ujumla kuchangia safari hiyo ili kuokoa maisha ya daktari huyo, huku akitaja namba za mawakala wa simu za Vodacom na Tigo, ambazo zitatumika kukusanya michango hiyo.

Habari zilizopatikana baadaye wakati tunakwenda mitamboni zilieleza kuwa, Dk Ulimboka alitarajiwa kusafirishwa kwenda Nairobi, Kenya kwa matibabu zaidi.


TANNA MOI watoa tamko
Katika hatua nyingine, Chama cha Wauguzi (Tanna), Tawi la MOI kilitoa tamko la kulaani kitendo cha kutekwa, kupigwa na kujeruhiwa kwa Dk Ulimboka na kutaka uchunguzi wa kina na haraka ufanyike ili kubaini watu waliohusika.

Mwenyekiti wa Tanna, Tawi la Moi, Prisca Tarimo alisema katika tamko hilo kuwa, kitendo alichofanyiwa Dk Ulimboka ni cha kinyama na kisicho cha kiutu.

Katika tamko hilo, Tanna imeomba Serikali kutafuta suluhu ya mgomo huo haraka kwa kuwa unaathiri maisha ya watu na kuwaongezea mzigo wa kiutendaji wauguzi.

Mgomo wa madakati unaingia siku ya saba leo, huku suluhu ya kuaminika ya kutatua tatizo hilo, ikiwa bado haijapatikana.

Polisi wakanusha
Katika hatua nyingine, James Magai anaripoti kuwa, Jeshi la Polisi limekanusha kumteka na kumjeruhi Dk Ulimboka, huku likipinga pia taarifa za daktari huyo kumtambua mmoja wa askari walio katika jopo la uchunguzi wa tukilo hilo alipokwenda kumtembelea hospitalini.

Pia jeshi hilo limetoa wito kwa madaktari hao walioko katika mgomo kuwa na busara na kutii amri ya Mahakama, ya kuwataka wasitishe mgomo wao.

Pia limeonya kuwa ikiwa wataendelea kukaidi na kupuuza amri ya hiyo ya mahakama, linao wajibu wa kuwachukulia hatua kwa kuwafikisha mahakamani, ili wajibu mashtaka hayo.

Msimamo huo ulitolewa jana na Kamishna wa Oparesheni Maalumu, Kamishna wa Polisi (CP), Paul Chagonja wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari kwenye mkutano alioitisha kuzungumzia matokeo ya operesheni ya jeshi hilo ya majuma matatu katika kuzuia uhalifu nchini.

Alisema madai hayo ni uvumi ambao unalenga kulifanya jeshi hilo lisiaminike na kufifisha juhudi zake za kuwasaka waliohusika na unyama huo.

Monday, May 28, 2012

MWACHENI MUNGU AITWE MUNGU!!


Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ akiwa hospitalini nchini India.
Sajuki akiwa amepumzika, pembeni ni mkewe Wastara Juma.

HEBU mwacheni Mungu aitwe Mungu! Hatimaye habari njema kutoka katika Hospitali ya Saifee iliyopo jijini Mumbai, India anakotibiwa staa wa filamu za Kibongo, Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ zinatia faraja kwa Watanzania, Ijumaa Wikienda linakupa stori ‘exclusive’ kutoka nchini humo.
ANYANYUKA KITANDANI, AONGEA
Habari hizo njema zinaeleza kuwa Sajuki aliyeambatana na mkewe, Wastara Juma na kaka yake, hatimaye ameweza kunyanyuka kitandani na kuongea tofauti na siku aliyoondoka Bongo na mwanzoni alipofikishwa hospitalini hapo.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, mwishoni mwa wiki iliyopita kwa njia ya simu, Wastara alisema Sajuki alikuwa amepata nafuu na hali siyo mbaya kwani alikuwa na uwezo wa kuzungumza hivyo akampa simu ili azungumzie afya yake yeye mwenyewe jinsi anavyojisikia.
SAJUKI LAIVU
Sajuki alipopewa simu alianza kwa kuwashukuru wale wote wanaomuombea dua na kujitolea kwa hali na mali ili kuokoa uhai wake.
“Namshukuru sana Mungu naendelea vizuri. Nilichukuliwa vipimo na nikabainika kuwa na uvimbe mwingi sehemu mbalimbali tumboni.
“Madaktari walibaini kuwepo kwa uchafu kwenye mapafu. Mwanzoni waligundua nina tatizo la kupumua na kukaukiwa damu.
“Wamelishughulikia hilo kwanza na hapa nilipo nimezungukwa na madawa, kwa kweli najisikia nafuu,” alisema Sajuki kwa sauti ya kukwaruza.
MADAKTARI
Sajuki alisema alipokelewa vizuri lakini kabla ya kuanza matibabu ya uvimbe tumboni, madaktari walilazimika kumtibu kwanza tatizo la damu na pumzi hivyo matibabu ya kilichompeleka hospitalini hapo (uvimbe) yakawekwa pembeni.
WASTARA ATIA NENO
Kwa upande wake, Wastara alisema kuwa Sajuki alipaswa kupatiwa matibabu kwa wiki mbili ndipo warejee nyumbani lakini kwa hali halisi inaonekana watakaa zaidi kwani tayari wiki mbili zimekatika.
MATIBABU YAANZA
Wastara alisema kuwa baada ya kumalizika kwa tatizo la pumzi na kupungukiwa damu, madaktari wameanza vipimo vya tatizo la uvimbe na kusisitiza kuwa uzi ni uleule wa kumwombea mumewe ili arejee katika siha njema.
TUMEFIKAJE HAPA?
Sajuki alianza kusumbuliwa na uvimbe mwaka jana ulioanzia mkononi na baadaye ndani ya mwili kwenye ini na sasa madaktari wanasema siyo kwenye ini tu bali na sehemu nyingine tofauti za tumboni.
NENO
Kama alivyosema Wastara, tuzidi kumuombea dua Sajuki ili arejee katika ulingo wa filamu aendelee kutuelimisha na kutuburudisha tunapokuwa majumbani mwetu.

Thursday, May 17, 2012

Baadaya Kanumba,Eeeh Mafisango Tena!!!Nani atafuata?


Rafiki wa karibu na marehemu ambaye amenusurika kwenye ajali hiyo (kulia) akilia kwa uchungu.
Mchezaji wa Simba, Haruna Moshi ‘Boban’ (kulia),  akiwa wamekaa kwa huzuni na  wenzake.
Boban akilia kwa uchungu.…

Rafiki wa karibu na marehemu ambaye amenusurika kwenye ajali hiyo (kulia) akilia kwa uchungu.
Mchezaji wa Simba, Haruna Moshi ‘Boban’ (kulia),  akiwa wamekaa kwa huzuni na  wenzake.
Boban akilia kwa uchungu.
Mchezaji wa Moro United, Jackson Chove, akiwa na huzuni.
Waombolezaji  ambao ni mashabiki zake wakilia kwa uchungu.
Kifo cha kiungo mkabaji wa timu ya Simba, Patrick Mafisango,  kilichotokea leo alfajiri maeneo ya Veta-Chang’ombe  jijini Dar es Salaam baada ya kupata ajali ya gari,  kimewahuzunisha watu  wengi ambao  walikusanyika nyumbani kwa mchezaji mwenzake, Emannuel Okwi, maeneo ya Bora-Keko ambako taratibu za msiba zinafanyika huku wakilia kama watoto.

40 ya Kanumba Giza latanda!!!


Marehemu Steven Charles Kanumba ‘The Great’.
Mama mzazi wa marehemu Kanumba, Flora Mtegoa.
Baba mzazi wa marehemu Kanumba, Mzee Charles Kanumba.…
Marehemu Steven Charles Kanumba ‘The Great’.
Mama mzazi wa marehemu Kanumba, Flora Mtegoa.
Baba mzazi wa marehemu Kanumba, Mzee Charles Kanumba.
Sehemu ya umati uliohudhuria msiba wa marehemu Kanumba.
Issa Mnally na Shakoor Jongo
LEO ni siku ya arobaini tangu kifo cha aliyekuwa nyota wa sinema za Bongo, Steven Charles Kanumba ‘The Great’ lakini giza nene linaonekana kuigubika shughuli hiyo kufuatia tamko la mama wa marehemu, Amani linakuja na habari kamili.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu juzi Jumanne, mama wa marehemu, Flora Mtegoa alisema ni kweli arobaini imefika lakini hajui kinachoendelea ila itafanyika Mei 20, 2012.
TAMKO LA MAMA
Mama Kanumba alikuwa akijibu swali la kipaparazi lililomtaka afafanue kama mkusanyiko wa arobaini ya marehemu utakuwepo au kila mtu atakuwa kivyake.
“Nimeambiwa itafanyika tarehe 20 mwezi huu lakini zaidi ya hapo sijui chochote kile kinachoendelea mwanangu,” alisema mama huyo kwa sauti iliyojaa unyenyekevu.
HABARI NDANI YA TASNIA YA SINEMA
Amani lilizungumza pia na mmoja wa wasanii wa filamu za Kibongo ambaye hakupenda jina lake liwekwe wazi. Yeye alikuwa na haya ya kusema:
“Ilibidi arobaini yake
ifanyike Mei 17 (leo) lakini kila tukiulizia tunaambiwa mipango bado haijakamilika, mipango gani hiyo kama fedha zilipatikana nyingi sana katika rambirambi.
“Wanaona hasara kuzitoa kwa ajili ya kununulia vifaa vya arobaini?”
Aidha, msanii huyo aliitaka kamati ya maandalizi ya arobaini hiyo (kama ipo) kutoifanya kienyeji na kushauri kuwa inabidi itangazwe ili watu wahudhurie kwa wingi kama siku ya mazishi.
“Kinachoonekana wanataka kufanya shughuli bora ifanyike, watakuwa wameharibu sana. Wakifanya shughuli kubwa pengine hata rais au mawaziri na wabunge wanaweza kuhudhuria,” alisema msanii huyo.
MANENO YA JB
Msanii Jacob Steven JB, Mwenyekiti wa Bongo Movie, alipoulizwa na gazeti hili siku ya Jumanne (juzi) alisema hajui lolote kuhusu arobaini hiyo.
Akasema: “Kwa taarifa nzuri labda muulize Gabriel Mtitu ‘Mtitu Game’ (aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Maziko), yeye atakuwa anajua lolote.”
SAUTI YA MTITU GAME
Amani lilimtwangia simu Mtitu Game na kumuuliza kama anajua lolote kuhusu kuwepo kwa arobaini ya marehemu Kanumba.
“Aaa, yeah! Arobaini imeangukia Alhamisi, siku ya kazi. Kwa hiyo familia ikaona ifanyike Mei 20, mwaka huu ambayo itakuwa Jumapili,” alisema Mtitu.
Amani: “Kwa hiyo ishu itakuwaje?”
Mtitu: “Aaa! Kutakuwa na ibada pale Kanisa la AIC Chang’ombe, halafu baadaye wanandugu watakusanyika nyumbani kwa marehemu (Sinza) kwa ajili ya chakula cha pamoja.”
Amani: “Hakuna mwito kwa mtu yeyote atakayetaka kuja?”
Mtitu: “Sijalijua hilo.”
BABA KANUMBA NAYE
Baada ya mawasiliano yote hayo, Amani lilimpigia simu baba mzazi wa marehemu, Mzee Charles Kanumba na kumuuliza kuhusu kuwepo au kutokuwepo kwa arobaini ya mwanaye.
Akafunguka: “Sijajua, ila lazima iwepo.”
Amani: “Huku mama wa marehemu naye anasema hajui lolote, wewe unasema hujajua.”
Baba: “Yeye (mama Kanumba) kusema hajui lolote ni janja ya nyani tu. Mimi najiandaa kuja huko siku mbili hizi, nikifika kila kitu kitajulikana.”
CHANZO CHA YOTE
Chanzo cha yote haya ni simu zilizoanza kumiminika kwenye Ofisi za Global Publishers, wasomaji wa Dar na mikoani wakiulizia shughuli hiyo itafanyikia wapi ili wahudhurie.
Juma Makala wa Mwanza, alitaka kujua siku na mahali ili aweze kufika baada ya kushindwa kuhudhuria mazishi ya marehemu.
“Jamani naitwa Juma Makala, niko Mwanza. Hivi hii arobaini ya Kanumba ni lini? Nahisi imekaribia. Na itakuwa wapi? Kwa sababu sikuweza kuhudhuria kwenye mazishi sasa nilitaka kujua ili niweze kufika.”
Amani lilimjibu aendelee kufuatilia magazeti ya Global atajua ni lini.
Mama Mage wa Kinyerezi, Dar yeye alisema alitaka kwenda Afrika Kusini kwa matibabu lakini amesitisha kusubiri arobaini ya Kanumba lakini hajui itakuwa lini.
Amani lilimuomba kuendelea kusoma magazeti ya Kampuni ya Global Publishers ili kujua ni lini na wapi.
NENO LA MHARIRI
Arobaini ya Kanumba imefika, kama ni Mei 20 ni vyema watu wakasubiri tamko maalum la familia ambalo naamini litaweka wazi hata wenye sifa za kuhudhuria.

Sunday, May 13, 2012

Man city bingwa England



Nahodha wa Manchester City, Vincent Kompany akiwa amenyanyua juu kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya England baada ya kuwafunga QPR katika mechi ya leo.Mshambuliaji wa  Manchester City, Sergio Aguero (jezi namba 16) akiifungia timu yake bao la tatu na la ushindi dhidi ya Queens Park Rangers katika mechi iliyopigwa leo kwenye Uwanja wa Etihad mjini Manchester, England. Manchester City wametwaa ubingwa wa Ligi Kuu England kwa tofauti ya mabao na Manchester United.
 (Picha zote kwa hisani ya Getty Images)…


Nahodha wa Manchester City, Vincent Kompany akiwa amenyanyua juu kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya England baada ya kuwafunga QPR katika mechi ya leo.Mshambuliaji wa  Manchester City, Sergio Aguero (jezi namba 16) akiifungia timu yake bao la tatu na la ushindi dhidi ya Queens Park Rangers katika mechi iliyopigwa leo kwenye Uwanja wa Etihad mjini Manchester, England. Manchester City wametwaa ubingwa wa Ligi Kuu England kwa tofauti ya mabao na Manchester United.
 (Picha zote kwa hisani ya Getty Images)

Thursday, May 10, 2012

KINACHOMTESA LULU!!





ITAKUMBUKWA kuwa Jumatatu iliyopita, mshitakiwa katika kesi ya kifo cha staa wa sinema za Kibongo, Steven Charles Kanumba ‘The Great’, Elizabeth Michael ‘Lulu’ alitupiwa ombi lake la kutaka mahakama imtambue kuwa ana miaka 17 badala ya 18 ili kesi hiyo iendeshwe kwenye mahakama ya watoto.

Kesi hiyo ambayo iliunguruma Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, mawakili wanaomtetea mshitakiwa huyo wakiongozwa na Kenedy Fungamtama waliwasilisha cheti cha kuzaliwa cha mlalamikiwa wao kinachoonesha ana miaka 17.
Hoja hiyo ilitupiliwa…



ITAKUMBUKWA kuwa Jumatatu iliyopita, mshitakiwa katika kesi ya kifo cha staa wa sinema za Kibongo, Steven Charles Kanumba ‘The Great’, Elizabeth Michael ‘Lulu’ alitupiwa ombi lake la kutaka mahakama imtambue kuwa ana miaka 17 badala ya 18 ili kesi hiyo iendeshwe kwenye mahakama ya watoto.
Kesi hiyo ambayo iliunguruma Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, mawakili wanaomtetea mshitakiwa huyo wakiongozwa na Kenedy Fungamtama waliwasilisha cheti cha kuzaliwa cha mlalamikiwa wao kinachoonesha ana miaka 17.
Hoja hiyo ilitupiliwa mbali na mawakili wa upande wa mashitaka waliokuwa wakiongozwa na mwendesha mashitaka mkuu wa mahakama hiyo, Elizabeth Kaganda ambaye alisema cheti hicho kina dosari kadhaa.
Naye hakimu aliyesikiliza kesi hiyo, Augustine Mmbando alisema mahakama hiyo itaendelea kuutambua umri alioutaja mshitakiwa wakati akitoa maelezo yake polisi hadi pale kesi yake itakapoanza kusikilizwa na Mahakama Kuu ya Tanzania.
DOSARI YA KWANZA
Jina la mshitakiwa lilisomeka ni Diana Elizabeth Michael badala ya Elizabeth Michael. Mwendesha mashitaka huyo alisema jina hilo ni geni mahakamani hapo.
DOSARI YA PILI
Kaganda alisema mapungufu mengine ni cheti hicho kugandishwa kwenye nailoni (lamination) jambo ambalo halitakiwi kwenye uhifadhi wa vyeti.

KINACHOMTESA LULU
Kwa mujibu wa mazungumzo ya watu na wanasheria kadhaa, Lulu kwa sasa anateswa na mazingira aliyokuwa akiishi ambayo kwa sehemu kubwa yanapingana na umri unaotajwa.
Endapo msanii huyo angekuwa si maarufu, hakuna mtu ambaye angeibua utata wa umri wake kwa vigezo au ushahidi kama ilivyo sasa.
Kwa mujibu wa Kaganda, wakati akitoa maelezo kwenye Kituo cha Polisi Oysterbay, Dar baada ya kukamatwa, Lulu alisema ana miaka 18 na aliambiwa ayapitie mara kadhaa maelezo yake kabla ya kuanguka sahihi.
Akizungumza baadaye, afisa mmoja mwandamizi wa mahakama hiyo alimwambia Kaganda:
“Wanasema Lulu ana umri wa miaka 17, mbona huwa anaonekana akiendesha magari, alipataje leseni akiwa na umri wa chini ya miaka 18?”
Kaganda: “Si ndiyo hapo sasa!”

SHEREHE YA BETHIDEI
Pamoja na malumbano hayo makali juu ya umri wa Lulu ndani ya mahakama hiyo, nje nako minong’ono ilishamiri. Sherehe yake ya kutimiza miaka 18 iliyoripotiwa kwenye vyombo vya habari, Aprili 2011 nayo ilitajwa.
“Halafu huyu Lulu si alishafanya bethidei ya kutimiza miaka 18 mwaka 2011, tena hata magazeti na kwenye mitandao waliandika,” alisema mtu mmoja nje ya mahakama hiyo.
“Nini kufanya bethidei, kwenye kipindi cha Mkasi alipohojiwa na Salma Jabir wiki moja tu kabla ya kifo cha Kanumba, Lulu alikiri ana miaka 18. Lakini pengine kweli, labda ni utoto ndiyo maana hana uhakika na umri wake,” alisema mwingine.

KUJIRUSHA KLABU
Aidha, minong’ono hiyo pia ilisikika ikijadili suala la msanii huyo kuwahi kuripotiwa (Machi 2011) kwamba alipigwa marufuku na mameneja wa klabu kubwa za usiku za jijini Dar kutokana na kuwa na umri mdogo, lakini baadaye mwenyewe akasema ‘amuone huyo wa kumkataza kuingia klabu.’
Wafuatiliaji hao walisema baada ya kutoa tamko hilo ndipo miezi michache mbele, Lulu akaangusha bethidei ya nguvu kwamba alitimiza miaka 18 hivyo alikuwa huru kuingia klabu kujirusha.
Walisema katika kujirusha kwake klabu, alisharipotiwa kuwa aliwahi kulewa chakari hadi nguo zikamvuka.

MADAI YA UHUSIANO NA ALI KIBA
Wapo pia waliokumbusha habari iliyowahi kuandikwa kwenye gazeti la Risasi la Septemba 4, 2010 ikiwa na kichwa cha kisemacho; ALI KIBA KUFIA JELA…endapo itathibitika Lulu ni mtoto mdogo (chini ya 18).
Katika habari hiyo, ilidaiwa kuwa, msanii huyo wa Bongo Fleva alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Lulu ambaye iliaminika ana miaka chini ya 18.
MAMA MZAZI ATETWA
Mama mzazi wa Lulu ameendelea kubebeshwa lawama kuhusu utata huo. Wengi walisema wakati mtoto wake anafanya bethidei kutimiza miaka 18 aliona au kusoma kwenye magazeti, kwa nini asipinge kama alijua amedanganya?
“Mama anasema mtoto wake ana miaka 17, siku zile anafanya bethidei mwanaye huyo alisema ametimiza miaka 18 kwa nini asipinge, ameona yaliyotokea sasa?” alihoji Mwantumu, mkazi wa Upanga, Dar.

MEZANI KWA MHARIRI
Amani linaamini yote ni maneno yanayosemwa, mahakama zetu zipo imara na zenye kufuata sheria, zitaendesha kesi hiyo kwa mujibu wa sheria na si maneno ya watu.

Wednesday, May 9, 2012

Mtoto Krish akifurahia jambo.
Muigizaji Tino akiwasha mishumaa.
Baadhi ya watoto yatima wakiimba wimbo wa ‘Happy Birthday’.
Krish na mama yake wakizima mishumaa.…
Mtoto Krish akifurahia jambo.
Muigizaji Tino akiwasha mishumaa.
Baadhi ya watoto yatima wakiimba wimbo wa ‘Happy Birthday’.
Krish na mama yake wakizima mishumaa.
Krish akisaidiwa na mama yake kukata keki.
Uwoya akimlisha kipande cha keki mtoto wake.
Uwoya akitoa hotuba.
Watoto yatima wakiwa na Uwoya, Mariamna Krish.
Uwoya akikabidhi msaada wake kwa katibu mkuu wa kituo hicho cha CHAKUWAMA.
ICON wa filamu nchini, Irene Uwonya jana usiku wa Mei 8 aliandaa bonge la siku ya kuzaliwa mtoto wake wa kiume, Krish Ndikumana, akiwa ametimiza umri wa mwaka mmoja tangu azaliwe.
Krish ni mtoto wa mwanasoka raia wa Rwanda, Hamad Ndikumana ‘Kataut’.

Sherehe hiyo ilifanyika katika kituo cha watoto yatima cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza-Mori jijini Dar.

Akizungumza na mtandao huu, mama wa mtoto huyo, Irene Uwoya, alisema amefarijika sana kufanya sherehe ya mwanaye akijumuika na watoto yatima kwani ameona ni moja ya kuwahakikishia watoto hao kuwa jamii inawajali.

“Sikutaka sherehe hii ya mwanangu niifanye katika ukumbi na kualika watu wengi ili waje kunywa na kula huku nyinyi watoto wenzake mkiwa mpo, kwani hiyo haitokuwa vizuri kwa upande wangu,” alisema Uwoya.


(by global publishers.)